Preetha Reddy, Makamu Mwenyekiti wa Hospitali za Apollo,

Na Mwandishi Wetu,
CHENNAI ni jiji la tano kwa ukubwa nchini India, jiji hilo limepigwa na janga kubwa la mafuriko ambayo hayajawahi kutokea kwa zaidi ya miaka 100 iliyopita, mafuriko hayo yameliacha jiji hilo likiwa hoi na taabani. 

Mafuriko hayo ya kihistoria yalisababisha jiji hilo kukosa huduma muhimu kama umeme, maji safi, chakula, usafiri na mahitaji mengine ya msingi. Idadi ya wagonjwa wengi wameripotiwa kufariki baada ya maji ya mvua kubwa kuharibu majenereta na mfumo mzima wa umeme kwenye hospitali mbalimbali mjini humo.

Kufuatia mafuriko hayo makubwa jiji Chennai, hospitali za Apollo zilizopo Chennai zimeripotiwa kuwa zinaendelea kufanya kazi vizuri na kuwa mstari wa mbele kutoa huduma kwa waathirika wote wa hayo mafuriko. Wakati hospitali nyingi Chennai zikiwa zinasumbuka na tatizo la umeme; hospitali za Apollo zina endelea kutoa huduma bora na kuzidi kutumia timu yao ya wataalamu waliojikita katika kuokoa maisha ya watu wengi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...