Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Sayansi na TekinolojiaPriska Olomi (kushoto) , akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam leo, kuhusu kutungwa kwa kanuni za huduma za ziada kwa makampuni ya simu nchini zitakazo walinda watumiaji wa huduma hizo,kulia ni Mkuu wa kitengo cha Sheria wa Wizara hiyo,Veronika Sudayi. 
(Picha na Hassan Silayo).

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KANUNI MPYA ZA HUDUMA ZA ZIADA ZA MWAKA 2015 ZA SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA YA MWAKA 2010 

(THE ELECTRONIC AND POSTAL COMMUNICATION ACT 2010 (VALUE ADDED SERVICES) REGULATIONS 2015) 

Ndugu Waandishi wa Habari 
1. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutupatia uhai na afya njema na kutuwezesha kukutana leo kupeana taarifa kuhusu Kanuni Mpya za Huduma za Ziada za Mwaka 2015 ambazo zinatokana na Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya Mwaka 2010. Napenda pia kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa kukubali mwito kushiriki nasi katika siku hii ya leo. Karibuni sana. 

Ndugu waandishi wa Habari.
2. Sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeendelea kukua kwa kasi duniani na hapa nchini kwetu na imeleta mafanikio mengi katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kijamii kwenye ngazi ya kitaifa na kwa mwananchi mmoja mmoja katika maisha ya kila siku kwa waishio mijini na vijijini. Idadi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano nchini imeendelea kuongezeka kutoka line za simu za viganjani milioni 2.96 mwaka 2005 hadi kufikia milioni 32.1 mwezi Desemba 2014. Watumiaji wa mfumo wa intaneti nao wameongezeka kutoka milioni 3.56 mwaka 2008 hadi kufikia milioni 11.34 mwaka 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...