Desemba 02,2015- Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameendelea na ziara za kushtukiza kwenye maeneo ambayo ni kero katika wilaya hiyo.Ilikuwa majira ya saa tano asubuhi,mkuu huyo wa wilaya akaabukia katika soko kuu la manispaa ya Shinyanga lililojengwa kabla ya uhuru wa Tanganyika..Ikawa faraja kwa Wafanyabiashara wa soko hilo waliodai kwa kipindi kirefu wamekuwa wakiilalamikia halmashauri ya manispaa kutokana na kushindwa kulifanyia ukarabati soko hilo.Akiwa katika soko hilo Josephine Matiro amesikiliza kero nyingi kutoka kwa wafanyabiashara hao ikiwemo ukosefu wa mitaro,kalo la maji,uchafu sokoni.Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo eneo la tukio..Anatusimulia kwa picha 40 kilichojiri mwanzo hado mwisho..Tazama hapa chini
Mkuu wa wilaya ya Shinyang Josephine Matiro akiwa na mwenyekiti wa soko kuu mjini Shinyanga Alex Stephen ambaye alisema kwa muda mrefu kumekuwa na kero ikiwemo ukosefu wa mitalo ya kupitishia maji machafu,kalo la maji machafu kujaa,ghuba la taka kujaa mara kwa mara.Alisema licha ya kwamba wataalamu wa halmashauri walishafanya tathmini ya namna ya kujenga mitaro lakini hakuna utekelezaji uliofanyika huku wao wakiendelea kupata kero wakati wanalipa ushuru na michango mingine inayohitajika.
Ndani ya soko kuu la manispaa ya Shinyanga viazi vikiwa chini pembeni maji machafu
Hili ni soko la manispaa ya Shinyanga/mkoa wa Shinyanga lililojengwa zaidi ya miaka 50 iliyopita
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...