MWANAFUNZI Evelina Edwin Kazaura (13), (pichani) wa shule ya msingi Dodoma mlimani, Manispaa ya Dodoma amepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Kwa mujibu wa mzazi wa mwanafunzi huyo, Joyce Nchimbi, alisema mtoto huyo alitoweka nyumbani miezi mitatu iliyopita akiwa amevaa nguo hiyo.

Alisema mara ya mwisho alionekana mitaa ya Railways akiwa na wanafunzi wenzake lakini baada ya hapo hajaonekana tena.

Joyce alisema juhudi za kumtafuta mtoto huyo kwa ndugu na jamaa hazikufanikiwa na kutoa taarifa katika kituo cha polisi cha kati Dodoma na kufunguliwa jalada namba DOM/RB/5005/2015.

Joyce ameomba kwa yeyote atakayemuona mtoto huyo atoe taarifa kituo chochote cha  polisi au apige simu namba 0756- 365064 au 0654- 666755.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...