Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni
ya PanAfrican Energy Andrew
Kangashaki (kushoto ) na Mkurugenzi
wa Wilaya ya Kilwa
Twalib Mbasha wakikabidhiana mkataba wa miradi ya ujenzi wa nyumba ya
mama ngojea katika hospital ya Kinyonga na ukarabati wa wodi ya
uzazi mara baada ya kumaliza kusaini mikataba hiyo katika hafla fupi
iliyofanyika jana Kilwa Kivinje.
Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni
ya PanAfrican Energy Andrew
Kangashaki(wa tatu kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa
Twalib Mbasha (wa tatu kulia) wakisaini makubaliano ya miradi miwili ya ujenzi
wa mama ngojea ‘maternity waiting home’ yaani nyumba maalum kwa kina mama
wajawazito watakaokua wakisubiri kujifungua itakayojengwa katika hospitali ya
Kinyonga – Kilwa Kivinje na kukarabati wodi ya uzazi na chumba maalum cha
uangalizi wa akina mama mara tu baada ya kujifungua katika kituo cha afya cha
Kilwa Masoko.
Huku wakishuhudiwa na Mwanasheria wa Wilaya Mh. Godfrey Makary (wapili kutoka kulia), Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Juma Abdalah Njwayo(wa pili kushoto), Mbunge wa jimbo la Kilwa Kaskazini kupitia chama cha CUF Mh. Vedasto Edgar Ngombale(wakwanza kushoto) pamoja na Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama cha CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wakwanza kulia).
Huku wakishuhudiwa na Mwanasheria wa Wilaya Mh. Godfrey Makary (wapili kutoka kulia), Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Juma Abdalah Njwayo(wa pili kushoto), Mbunge wa jimbo la Kilwa Kaskazini kupitia chama cha CUF Mh. Vedasto Edgar Ngombale(wakwanza kushoto) pamoja na Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama cha CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wakwanza kulia).
Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama cha
CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wapili kulia) akitoa neno la shukrani kwa
Kampuni ya PanAfrican Energy kwa niaba ya wananchi wa Kilwa Kusini mara baada
ya makabidhiano ya mkataba wa miradi itakayowanufaisha wananchi wa kilwa.
Wafadhili wa mradi wa ujenzi wa wodi ya
wazazi Kampuni ya PanAfrican Energy pamoja wakiwaonesha wanahabari chumba cha
uzazi katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko ambacho kipo katika mradi uliosainiwa
kati ya wilaya ya Kilwa na kampuni hiyo. Hii ni katika kuunga jitihada za
serikali za kuboresha huduma za afya.
Hali
halisi ya mazingira ya wodi ya wagonjwa katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko,
hii ni wodi ya wanaume. Kiyuo hichi cha afya
kilijengwa mwaka 1952 enzi za ukoloni mpaka sasa hakijawahi
kukarabatiwa.
Wauguzi
wa Hospitali ya Kinyonga Kilwa Kivinje wakishuhudia makabidhiano ya mkataba wa
miradi ya ujenzi wa mama ngojea ‘maternity waiting home’ utakaofanyika katika
hospitali yao na mradi mwingine wa ukarabati wa wodi ya uzazi utakaofanyika
katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo
jana.PICHA NA MICHUZI JR-MICHUZI MEDIA GROUP.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...