Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi, (wakwanza kulia), akiungana na Mbunge wa viti maalum, Angela Kairuki, (wapili kulia), mkurugenzi w manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, Photidus Kagimbo, watatu kulia), mganga mfawidhi wa hospitali ya Temeke, Dkt. Amani Malima, (wane kulia) na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Temeke, Dkt. Sylvia Mamkwe, (wakwanza kushoto), wakati PSPF, ikikabidhi msaada wa vitanda, mashuka na magodoro kwa hospitali hiyo, Desemba 7, 2015. Msaada huo ni utekelezaji wa ahadi ya Mfuko baada ya kuombwa na Mh. Angela Kairuki.

Mbunge wa viti Maalum, Angella Kairuki, (wapili kulia), akipokea msaada wa vitanda, kutoka kwa Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, kwenye hosptali ya Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Desemba 7, 2015. Mfuko huo umetoa msaada wa vitanda, magodoro na mashuka ili kuunga mkono juhudi za serikali za kumaliza tatizo la vifaa tiba kwenye hosipatli za umma. Kulia ni .. Muuguzi mwandamizi wa hospitali hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...