Remija Salvatory na Nuru Mwasampeta

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo amewaagiza    Madaktari wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama kuandaa utaratibu wa kuwawezesha  wahanga wa  Mgodi wa Nyangalata  kwenda Hospitali za rufaa   kwa ajili ya uchunguzi  zaidi wa afya zao.

Mhandisi Chambo aliyasema hayo alipowatembelea wahanga hao waliolazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama  kutokana na ajali ya kufukiwa na kifusi na kufanikiwa kuokolewa baada ya kuishi chini ya ardhi kwa siku 41 katika Mgodi wa Nyangalata mkoani Shinyanga.

Katibu Mkuu alitoa maagizo hayo baada ya mmoja wa wahanga hao, Joseph Buruge kueleza kuwa ingawa ngozi za wachimbaji hao zinaonekana kuimarika   lakini bado kuna tatizo la  vijipele vidogo vidogo mwilini ambavyo baada ya muda hutoa usaa hivyo aliomba uchunguzi wa kina ufanyike ili kutibu tatizo hilo.

“Kwa kweli Mheshimiwa tunaendelea vizuri  na matibabu na tunawashukuru madaktari na wauguzi wote wanaotuhudumia na tunaishukuru Wizara na Serikali kwa ujumla  kwa misaada na huduma walizotoa, lakini kwa sababu umekuja Mheshimiwa  tuna maombi yetu ambayo tunaomba Serikari iweze kutusaidia sisi wahanga wote” , alisema Buruge.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...