Remija Salvatory na Nuru Mwasampeta
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo amewaagiza Madaktari wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wahanga wa Mgodi wa Nyangalata kwenda Hospitali za rufaa kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa afya zao.
Mhandisi Chambo aliyasema hayo alipowatembelea wahanga hao waliolazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama kutokana na ajali ya kufukiwa na kifusi na kufanikiwa kuokolewa baada ya kuishi chini ya ardhi kwa siku 41 katika Mgodi wa Nyangalata mkoani Shinyanga.
Katibu Mkuu alitoa maagizo hayo baada ya mmoja wa wahanga hao, Joseph Buruge kueleza kuwa ingawa ngozi za wachimbaji hao zinaonekana kuimarika lakini bado kuna tatizo la vijipele vidogo vidogo mwilini ambavyo baada ya muda hutoa usaa hivyo aliomba uchunguzi wa kina ufanyike ili kutibu tatizo hilo.
“Kwa kweli Mheshimiwa tunaendelea vizuri na matibabu na tunawashukuru madaktari na wauguzi wote wanaotuhudumia na tunaishukuru Wizara na Serikali kwa ujumla kwa misaada na huduma walizotoa, lakini kwa sababu umekuja Mheshimiwa tuna maombi yetu ambayo tunaomba Serikari iweze kutusaidia sisi wahanga wote” , alisema Buruge.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...