Mwanamuziki Kasongo Mpinda Clayton (anayeimba) ametutoka leo jioni baada ya kuugua kwa muda mrefu. Kasongo atakumbukwa kama mwimbaji mwenye sauti ya kipekee toka alipoibukia ghorofa ya saba pale New Africa Hotel jijini Dar es salaam akiwa na MK Group, wana Ngulupa Tupa Tupa na baadaye Maquis du Zaire 'Wana Kamanyola' akikonga nyoyo washabiki wa muziki, na baadaye Wazee Sugu chini ya King Kikii. 
Badhi  ya nyimbo zilizompandisha chati Marehemu Kasongo ni 'SEYA' , 'ANGELOU', 'MUME WANGU MWENYEWE'  na 'NSONONEKA' katika mtindo wa 'Ogelea piga mbizi' . Cheza hizo video nne umsikie Kasongo Mpinga....
Marehemu Kasongo anatarajiwa kuzikwa kesho saa 10 Kinondoni. Msiba upo nyumbani kwake Kinondoni karibu na jengo lenye Benki ya Akiba Commercial Bank jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Rajiuun.

    ReplyDelete
  2. Dah......chozi lanidondoka , R.I.P LEGENDARY

    ReplyDelete
  3. RIP Kasongo Mpinda. Hizi nyimbo nilikuwa nazikia sana nilivyokuwa mtoto ila nilikuwa sijui mwimbaji ni nani. Asante sana kwa kunikumbusha mbali. Naimisi RTD kipindi cha jambo na mchana mwema bila kasahau chaguo lako na club raha leo shooo! Na wakati umewadia wa salamu za wagonjwa hosipitalini leo tunawapa pole. Ajuae bwana Mungu kwa mzima kuwa mfu mgonjwa kuwa salama leo tunawapa pole. Dah!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...