Washiriki wa warsha hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na mwakilishi wa mgeni rasmi ambaye ni mshauri wa mradi huo Bw. Ahmed Athumani.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Soko la Ajira ,Mipango na Maendeleo wa VETA, Ahmed Athuman akizungumza katika warsha ya wadau wadau wa viwanda,umeme na magari kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati VETA na wadau hao iliyofanyika katika ukumbi wa Giraffee Hoteli jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wadau wakifatilia maada mbalimbali katika kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati VETA na wadau hao iliyofanyika katika ukumbi wa Giraffee Hoteli jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)imekutana na wadau wa viwanda,umeme na magari kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati yake na viwanda.

Akizungumza na wadau wa mamlaka hiyo wakati akifungua warsha hiyo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Soko la Ajira ,Mipango na Maendeleo wa VETA, Ahmed Athuman alisema moja ya sababu zinazokwamisha ajira kwa vijana nchini ni ukosefu wa mafunzo ya vitendo kwa vijana wanaohitimu katika taasisi mbalilmbali unaosababishwa na kutokukwepo kwa ushirikiano thabiti kati ya Taasisi za Mafunzo na Viwanda.

Amesema kuwa VETA inatoa mafunzo yatakayomuwezesha muhitimu kuajiriwa au kujiajiri kutokana na mafunzo ya vitendo yanayotolewa kutokana na mahitaji yaliyopo nchini 


Ahmed amesema kuwa ushirikiano wa wadau utaleta matokeo chanya kwa vijana kuweza kufanya kazi kutokana mafunzo walioyapata katika taasisi za mafunzo ya ufundi Stadi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mdau wa MaguDecember 01, 2015

    Warsha Tena? Haya mie simo.

    ReplyDelete
  2. He..hapo si ni Giraffe Hotel!? VETA hakuna kumbi na madarasa ya kutosha kukutana na Wadau!?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...