Na Krantz Mwantepele .Kahama
Wanawake ni nguzo muhimu sana katika uchumi wa watanzania wengi. Mwanamke ana ushawishi mkubwa na hasa pale anapoamua kuwa chachu ya maendeleo. Na hasa anapowezeshwa kufanya hivyo.
Katika kufanikisha hili waraghbishi wameamua kutoa mafunzo ya uraghbishi kwa makundi mengine ya jamii. Mojawapo ya kundi hilo ni la wanawake. Waraghbishi wapya toka katika kijiji cha Nyandekwa, kati ya hao wapo 9 ambao ni wanawake.
Mmoja wao ni Anna Alphonce, Mwenyekiti wa kitongoji cha Busolo, katika kijiji cha Nyandekwa. Akielezea jinsi alivyoanza uraghbishi alisema:
“Mi niliona kuna kikundi wanakaaga humu karibu kila jioni. Na kila nilipokuwa napita jirani na hapa naona watu wamejaa, basi nikapenda namimi nijiunge nao na hasa baada ya kujua nini wanafanya. Na hapo ndipo nilipoanza uraghbishi,”
Anna Alphonce (katikati) ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Busolo akifafanua jambo wakati akielezea uraghbishi anaofanya .
Akiwa kama mwenyekiti mwanamke wa kitongoji aliweza kutumia nafasi yake kufanya uraghbishi kwa anaowaongoza. Kwa kuwa kilikuwa ni kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu, aliitisha mikutano kwenye kitongoji chake kwa lengo la kutoa hamasa ya wananchi kujitokeza kwa wingi. Kwa nafasi yake aliweza kuyafikia makundi ya wazee, vijana na wanawake. Ingawa kati ya hawa wanawake ndio walikuwa washiriki wazuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...