Na Mwandishi Wetu
MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umeamua kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano, John Magufuli la kufanya usafi nchini siku ya sherehe za Uhuru 9/12/2015 kufagia, kulima, kuzoa taka na kusafisha maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana Dar es Salaam kuwa usafi huo utaanzia makao makuu yao Ilala Bungoni, soko la Ilala,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mmachinga Complex, Soko la Mitumba Karume, Kariakoo, Mnazi Mmoja, Soko la Kisutu, Posta ya zamani, soko la samaki Feri mpaka Ikulu.
Alisema zaidi ya wanachama 300 wa SHIWATA kutoka fani mbalimbali za wanamichezo, wasanii, waandishi wa habari na wadau wamethibitisha kushiriki kufanya usafi huo kutokomeza ugonjwa wa kipundupindu unashika kasi katika maeneo ya jiji la Dar es Salaam.
Taalib alisema kazi ya usafi huo itaanza saa 1.30 asubuhi kila mmoja aje na fagio, jembe, reki, au zana yeyote ya kufanyia usafi na kuvaa mavazi rasmi ya kufanyia kazi za usafi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...