Meza kuu,wa kwanza kulia ni Meneja wa redio PANGANI FM Maimuna Msangi, wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA ambalo limeratibu tamasha hilo VERA PIEROTH,wa tatu ni Kaimu mgeni Rasmi ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya PANGANI Bi Patricia, na wanne ni Mratibu wa masuala ya UKIMWI wilaya ya PANGANI.

Na Mwandishi wetu

Shirika lisilo la kiserikali Wilayani Pangani la UZIKWASA linalojishughulisha na kuziwezesha kamati za kudhibiti Ukimwi, VMACK limezawadia kamati bora za kudhibiti ukimwi Wilayani humo.

Sherehe hizo zimefanyika sanjari na kuwazawadia kijana bora mfano wa kuigwa na mama bora mfano wa kuigwa.

Katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Jaira,K ata ya Madanga wilayani Pangani na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wananchi na viongozi kutoka halmashauri ya Wilaya ya Pangani mgeni rasmi alikuwa Kaimu Afisa Maendeleo Wilaya ya Pangani, Bi.Patricia Kinyange.

Akizungumza katika hadhara hiyo Bi. Kinyange amelipongeza shirika hilo kwa kuzijengea uwezo kamati hizo ambazo zinafanya kazi kubwa kwa jamii.
 
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA, VERA PIEROTH akizungumza jambo wakati wa kuwakaribisha wananchi wa PANGANI katika tamasha hilo.


“Kwa kweli shirika la UZIKWASA nawapongeza sana, mnafanya kazi kubwa kwenye jamii ya Pangani na kwakweli watu wa Pangani wanapaswa kujivunia uwepo wenu. Nimeshangaa kuona mambo makubwa yanayofanywa na kamati kutokana na elimu mnayowapatia,mnastahili pongezi kubwa”alisema Bi.Kinyange.

“Mfano mzuri mimi ARUSHA nilipokua nafanya kazi, kamati zipo lakini kwakweli wamelala,unakuta kamati inakutana mara mbili kwa mwaka mzima,lakini huku ni zaidi ya mara kumi,kwakweli nimeshangaa sana,nyinyi ni shirika ambalo linafaa kuigwa,lakini wanakamati niwaombee mzidishe juhudi msiwaangushe wanauzikwasa na sisi kama halmashauri tutajitahidi kushirikiana kwa karibu kabisha na UZIKWASA ili kuendeleza juhudi hizi.”

Katika hatua nyingine mgeni huyo rasmi amempongeza kijana aliyeibuka mshindi katika shindano la kijana bora mfano wa kuigwa na kumtaka kuendeleza juhudi zake na kwamba Halmashauri watamtumia kama darasa kwa ajili ya vijana wengine kujifunza kutoka kwake.
 
Burudani ya ngoma ilikua sehemu ya tamasha hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...