Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Jumanne Sagini wakati akizungumza na watendaji mbalimbali wa ofisi hiyo leo katika mkutano wa kikazi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Karimjee jijini Dares Salaam , ambapo lengo kuu lilikuwa ni kutoa maelekezo ya utendaji kazi kama ilivyoagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa.Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Afya -TAMISEMI ,Dkt .Deo Mutasiwa .
Baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) wakimsilikiza Katibu Mkuu wa ofisi ambaye hayupo pichani.
Na Magreth Kinabo – maelezo
SERIKALI imewataka watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kuhakikisha kwamba wanafanyakazi kwa uadilifu weledi wa taaluma zao na kufuata sheria zilizopo katika kusimimia suala la usafi wa mazingira, likiwemo la kudhibiti biashara holela, gereji bubu,uegeshaji wa magari holela.
Pamoja na hayo wasimamie, upigaji holela wa muziki katika vilabu, baa na kumbi zaidi ya saa zilizopangwa na kuzuia bodaboda zinazosafirisha abiria hadi maeneo ya miji katikati, pia kuzuia ujenzi holela.
Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Jumanne Sagini wakati akizungumza na watendaji mbalimbali wa ofisi hiyo katika mkutano wa kikazi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Karimjee, jijini Dar es Salaam ambapo lengo kuu lilikuwa ni kutoa maelekezo ya utendaji kazi kama ilivyoagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa.
Akizungumzia kuhusu suala la usafi wa mazingira kufuatia ziara iliyofanyika hivi karibuni imeonekana kuwa na changamoto mbalimbali alisema;
Keep it up Permanent Secretary-PO RALG this order once implemented will make our cities good place to live. So now it up on CD, MDs to realize orders
ReplyDelete