Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa ,Balozi Augstine Mahiga amesema eneo la Laki Laki lililopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha lililotengwa kwaajili ya ujenzi wa taasisi za kimataifa utaifanya Tanzania kung'ara duniani.

Balozi Mahiga alisema hayo Desemba 19 baada ya kufanya ziara kwenye eneo hilo na Kituo cha mikutano cha kimataifa cha AICC .

Eneo hilo litajengwa Mahakama ya Kimataifa ya Kimbari(MICT)Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR) na taasisi zingine na kusema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa.

Akiwa kwenye kituo cha AICC alipokea taarifa za mradi wa ujenzi wa kituo cha mikutano cha kimataifa cha Kilimanjaro International Convention Center kitachovuta dunia Tanzania.

Pia Waziri alizungumzia hali ya kisiasa nchini Burundi kuwa inaigusa Tanzania na kuwa atawasiliana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC)Dk Richard Sezibera kuandaa kuandaa mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje.
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa,Balozi Augustine Mahiga(kulia)akiwasili kwenye kituo cha mikutano cha kimataifa cha Arusha International Conference Center(AICC) ambacho ni sehemu ya Wizara hiyo,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa AICC,Elishilia Kaaya. 
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa,Balozi Augustine Mahiga akizungumza na wajumbe wa Bodi ya AICC na watumishi wa kituo hicho ,kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya AICC,Balozi Christopher Lihundi na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Wilson Kambaku.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Arusha International Conference Center(AICC)Elishilia Kaaya akifafanua jambo mbele Waziri Mahiga(wa pili kulia)wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Wilson Kambaku(kulia)Mwenyekiti wa Bodi ya AICC,Balozi Christopher Lihundi(aliyevaa tai) na Mkuu wa mawasiliano serikalini,Mindi Kasiga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...