Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) na Naibu Waziri wa Wizara ya Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China, Wang Jiang wakisaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika masuala mbalimbali ya Ulinzi na Usalama wa Raia kati ya Wizara hizo mbili, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto), wakibadilishana Hati za Makubaliano ya Ushirikiano waliosaini na Naibu Waziri wa Wizara ya Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China, Wang Jiang, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto), akimpa zawadi ya kinyago Naibu Waziri wa Wizara ya Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China, Wang Jiang, mara baada ya kusaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano kati ya wizara hizo mbili. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto), akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China, Wang Jiang, mara baada ya kusaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano kati ya Wizara hizo mbili. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (wa pili kushoto), akimfafanulia jambo Naibu Waziri wa Wizara ya Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China, Wang Jiang (kulia), kabla ya kusaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano kati ya Wizara hizo mbili. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Katibu Mkuu, Mbarak Abdulwakil. Picha na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (watano kulia-mstari wa mbele), Naibu Waziri wa Wizara ya Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China, Wang Jiang (watano kushoto-mstari wa mbele), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (watatu kulia-mstari wa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mawaziri hao kumaliza kusaini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano kati ya wizara hizo mbili. Tukio hilo lilifanya katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...