Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na  Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Palestina hapa nchini, Mhe. Hazem Shabat. Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 30 Desemba, 2015.
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Balozi Mteule wa Palestina nchini, Mhe. Shabat mara baada ya kupokea nakala za hati  za utambulisho wake. Katika mazungumzo yao Balozi Shabat alimpongeza Waziri Mahiga kwa kuteuliwa kwenye wadhifa huo na kumuahidi ushirikiano. Pia Waziri Mahiga alimkaribisha nchini Balozi Shabat na kumuomba aendeleze mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Palestina.
Balozi Mteule wa Palestina nchini, Mhe. Shabat naye akizungumza huku Mhe. Dkt. Mahiga akimsikiliza.
Balozi Mteule Mhe. Shabat akimkabidhi Mhe. Mahiga zawadi ya picha inayoonesha Kanisa  lililopo katika mji wa  Jerusalem
Picha ya pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...