Kampuni ya
simu ya Zantel leo imetangaza kuzindua ofa maalumu kwa ajili ya msimu wa sikukuku
yenye lengo la kuwazawadia wateja wake muda wa maongezi bure na nyongeza ya asilimia 20% katika kila
manunuzi ya vifurushi au muda wa maongezi wanayofanya kupitia huduma ya
Ezypesa.
Ofa hii pia itamzawadia kila mteja wa Zantel anayefanya manunuzi ya muda
wa maongezi usio chini ya shillingi elfu moja kuweza kupata dakika za bure za
kupiga Zantel kwenda Zantel siku za mwisho wa wiki.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa
Zantel, Benoit Janin alisema ofa hiyo ni maalumu kwa ajili ya msimu huu wa
sikukuku yenye lengo la kukuza ubora wa huduma na kuwapa wateja fursa ya kufurahia huduma za mtandao
huo.
“Katika msimu huu wa sikukuku tumewazawadia wateja wetu ofa hii maalumu
ili iwasaidie kutumia kiasi kidogo katika kufanya mawasiliano na ndugu,jamaa na
marafiki kwenye msimu huu wa kusherekea sikukuu’
alisema Janin.Zantel kwa sasa imejikita zaidi katika kukuza na kuboresha huduma zake
na kuhakikisha inaboresha maisha ya jamii ya watanzania.
"Zantel
pia imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha inawafikia wateja wake na pia kukidhi mahitaji yao ya kimawasiliano, kwa
kuboresha huduma zake huku ikitoa ofa zaidi zenye kusisimua kwa mwaka 2016
'alisema Janin.
Ofa
hii imezinduliwa leo, ikiwa ni wiki moja tu toka bodi ya wakurugenzi wa Zantel
ilipotangaza kuzindua mtandao mpya wa 4G kwa Zanzibar pamoja na kuimarisha huduma
za kimawasiliano za mtandao huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...