Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Sellasie Mayunga akikabidhi ofisi mbele ya waandishi wa habari leo katika Makao Makuu ya Wizara, Dar es Salaam ambapo amemshauri Naibu Katibu Mkuu mpya DKT. Moses Kusiluka kushughulikia kwa ukaribu suala la mpaka wa Kimataifa wa eneo la Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi kutokana na jambo hilo kuwa na maslahi makubwa ya Taifa.
Pia, amemsahuri Naibu huyo kutoa kipaumbele kwa ujenzi wa kituo cha kupokea picha za anga (Satellite receiving station) kilichopangwa kujengwa nchini mkoani Dodoma ambapo pamoja na faida zingine kitarahisisha utoaji wa hati za hakimiliki za ardhi kimila.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...