Usimshauri  mtu  kuhusika  katika  kitendo chochote  ambacho  kinakatazwa  na  sheria. Kufanya  hivyo  kutakufanya  nawe  kuhesabika  umehusika katika  kosa  hilo. Hii  ni  hata  katika  mambo  ya  kawaida  tuliyozea.  
Ukimsikia  mtu  anapanga  kwenda  kumkomesha  fulani kwa  kumpa  kipigo  usitie  neno  lako labda  kama  unamzuia. Usijaribu  hata  kusema  nenda  kamfanyie  amezidi.  Maneno  hayo  ni  machache  lakini  kisheria  yatachukuliwa  kama  ushauri  kwa mtenda  kosa.
Au  mtu  anakwambia  nakwenda  kumpa  vidonge  vyake  kwa  maana  ya  kumtukana na  kumdhalilisha  na  wewe  unasisitiza kwa  kumwambia  ndio kampe  maana  amezidi, utakuwa  nawe  umeingia  kwenye  kosa  bila  kujali  ulienda  huko  lilikotokea  tukio au  haukwenda . Hizi  ni  jinai  za  kila  siku  ambazo  watu  hujikuta  wameingia  bila  kujua  na  wakifikishwa  vituo vya polisi  huanza  kulaumu kuwa  wameonewa kwa kuamini hawakutenda. Jihadhari. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...