Kivuko cha mto Kilombero mkoani Morogoro kimezama kikiwa na abiria zaidi ya 30 na magari yapatayo matatu

Habari kutoka Kilombero zilizothibitishwa na mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Bw. Leph Gembe zinadai kuwa ajali hiyo imetokea jana Majira ya saa 1 usiku wakati kivuko hicho kikitokea Ulanga.

Alisema kuwa Jumla ya watu zaidi ya 30 ndio walikuwepo katika kivuko hicho na kuwa jitihada za uokoaji zilifanyika na watu zaidi 29 waliokolewa

Alisema chanzo cha ajali hiyo ni upepo Mkali na mawimbi makali yaliyopelekea kivuko hicho kuzama na kuwa hadi sasa bado taarifa kamili kupatikana na pindi atakapopata habari kamili atazitoa

Mkuu huyo alisema kwa sasa yupo jijini Dar es Salaam kwa matibabu.
Muonekano wa Misingi ya Daraja la Mto huo, huku kivuko kilichozama kikionekana kulia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...