Na  Bashir  Yakub
Kawaida  serikali  hutwaa  maeneo. Huhamisha  wahusika  wamiliki  na  kuchukua  eneo  kwa  malengo  maalum  yaliyokusudiwa. Yaweza  kuchukuliwa  nyumba yako, kiwanja,au  hata  shamba. Mara  kadhaa  serikali  hufanya  hivi  panapo  mahitaji  maalum  ya shughuli  za  umma  kama  ujenzi  wa  miundombinu  kama  barabara  reli, huduma za  umeme  na  maji,  ujenzi  wa  shule vyuo, vituo  vya  afya  na  miradi  mingineyo  kwa  manufaa  ya umma.

1.FIDIA  YA  ARDHI NI NINI...
Fidia  ya  ardhi  ni  stahili  ambayo mwenye  ardhi  mmiliki  anatakiwa  kupata  pale  ambapo  ardhi  yake  inatwaliwa/inachukuliwa  na  serikali  kwa  matumizi  maalum  ya  serikali/umma.

2.  JE UNAWEZA  KUIKATALIA  SERIKALI   ARDHI  YAKO  ISICHUKULIWE ? 
Serikali  inapotaka  kumhamisha  mwananchi na  kuchukua ardhi  yake kupisha mradi wa umma  kisheria  mwananchi   hana  uwezo  wa  kukataa. Hii  ni  kwasababu  ardhi  yote  ni  mali  ya  umma  ambayo  mdhamini  wake  mkuu  ni  serikali kupitia  mamlaka  ya  rais. 
Hivyo  tunaweza  kusema  kuwa  ardhi  ni  mali  ya umma inayodhaminiwa na Serikali/Rais.
Kwa  hiyo  mwananchi  hawezi  kuikatalia  serikali kuchukua  mali   hiyo  isipokuwa  kisheria  ni  kuwa  anayehamishwa  apewe  fidia.  
Hata  ukiamua  kwenda  mahakamani  kupinga  kutwaliwa  ardhi  hautapinga  kuwa  serikali  isichukue  ardhi yako  kabisa, isipokuwa  utapinga  kuhusu  fidia,  labda  fidia  ndogo  au  utaratibu  mbovu  uliotumika  kukadiria  fidia, riba n.k.

Labda  kuwe  na  uonevu  au  hila  katika  kutaka  kutwaliwa  ardhi  yako  au namna  nyingineyo  ya  nia  ovu  ndipo  unaweza  kupinga  ardhi  yako  kutwaliwa.  Lakini  haitawezekana  kupinga  hatua  hiyo  ikiwa  kuna  malengo  maalum  ya  kutwaa  ardhi  kwa  ajili  ya  shughuli  za  umma.  Kusoma zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...