Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akizungumza na Bi. Ester Maganga aliyekatwa kidole na watu wenye imani potofu alipomtembelea nyumbani kwake kumjulia hali na kumpa pole ya kupoteza kidole chake, katika kijiji cha Mlalo Wilayani Lushoto. Januari 5,2016.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akitoa pole kwa Bi. Ester Maganga baada ya kukatwa kidole chake na watu wenye imani potofu katika eneo la Mlalo Wilayani Lushoto Tanga, tarehe 5 Januari, 2016.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi (katikati mwenye miwani) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali wa Wilaya ya Lushoto alipomtembelea Bi. Ester Maganga (kushoto kwake) aliyefanyiwa tukio la kikatili la kukatwa kidole na watu wenye imani potofu.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akipanda mche wa mparachichi nje ya makazi ya Bi. Ester Maganga (hayupo pichani) aliyefanyiwa ukatili wa kukatwa kidole ikiwa ni sehemu ya ukumbusho wa ujio wa Naibu Waziri.Tarehe 5, Januari, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Hongera zangu waziri AP kwa kuonyesha mfano wa namna viongozi wanavyoweza kupanda miti bila ya kutumia mabusati au mikeka. Viongozi wengi huonyesha tofauti kwa kuogopa kuchafuka hivyo kukanyaga mikeka wakati wanapanda miti. Jaribuni kuwa wakawaida.
ReplyDelete