WANANCHI wa mikoa mbalimbali wamejitokeza kuiomba kkampuni ya Msama Promotions ianzie Tamasha la Pasaka mikoa kwao mwaka huu huku wakazi wa dare s salaam wakisisitiza libaki mkoani humo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama ameliambia Gazeti hili kuwa, tayari amepokea maombi toka kwa wananchi na mashabiki wa mikoa ya Morogoro, Mwanza, Mbeya, Dodoma na Dar es Salaam wakitaka tamasha hilo lianzie kwao mwaka huu.

“Kamati yangu  inafuata taratibu za Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambazo ni pamoja na kupata kibali cha kufanikisha kufanyika kwa Tamasha hilo linaloshirikisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa Injili  wa ndani na nje ya Tanzania,” amesema Msama.

Salum Ismail Hamad ambaye ni mdau mkubwa wa Tamasha la Pasaka amesema anawaomba waandaaaji wa Tamasha hilo kutoliondoa jijini Dar es Salaam kwa sababu ni mkoa unaohusisha idadi kubwa ya mashabiki wa muziki wa Injili.

Rukia Joseph wa Kimara Dar es Salaam, alisema yeye anawapigia magoti waandaaji  kutoliondoa tamasha hilo jijini  Dar es Salaam hasaa kwa waimbaji wa nje ya Tanzania kama Solly Mahlangu na wengineo toka nje ya nchi.


Michael Deogratius alisema  ni ngependa Tamasha la Pasaka lihamie mikoani  kwa sababu ya ukubwa na umuhimu wa tamasha hilo ambalo linatimiza miaka 16 tangu kuasisiwa kwake.Msama alisema bado wanasubiri taratibu za kufanikisha tamasha hilo  kutoka Basata, hivyo nawaomba wakazi wa mikoani kuvuta subira wakati wakijiandaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Peleka tamasha la Pasaka 2016 mkoani TABORA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...