Mtu mmoja Jijini Mbeya (PICHANI JUU) ambaye hakuweza kutambulika kwa Majina,inadaiwa amekutwa amefariki  leo asubuhi kwenye moja ya uchochoro  wa nyumba zilizopo katika mtaa wa Mwamfupe.

Kifo cha Mtu huyo ambaye inaelezwa ni kijana wa makamo alikutwa amefariki kwenye uchochoro wa nymba hiyo mara baada ya kubainika na baadhi ya Wananchi,waliokuwa wakikatiza mtaa huo kuelekea mtaa mwingine,Baadhi ya Mashudhua wa eneo hilo wameeleza kuwa mtu huyo si mkazi wa mtaa huo,

 "Mtu huyo si Mkazi wa Eneo hili, bali Jioni ya jana waliomuona maeneno hayo akiwa katika hali ya kupepesuka Pepesuka kotokana na kunywa Pombe, na huenda hicho ndicho kilicho pelekea Kifo chake kwani hakuwa mwenye afya njema." Alibainisha mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo wakati akihojiwa na Mwandishi wa Globu ya Jamii iliofika eneo la tukio
Baadhi ya Wanachi wa Mtaa wa Mwamfupe wakijadiliana jambo katika eneo la  tukio.
Huzuni  ikatawa Eneo hilo.
Baadhi ya Wanachi sambamba na Wenyenyumba zilizo zunguka Eneo hilo la Tukio wakisubiri msaada kutoka Jeshi la Polisi.Globu ya Jamii inafuatilia taarifa kamili kutoka kwa jeshi la Polisi mkoani Mbeya.

\Picha na Fadhiri Atick - Mr.Pengo wa Globu ya Jamii-Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Sio wote wanaopepesuka wamelewa pengine kaleweshwa au kupewa kitu cha sumu na kushushwa hapo wafanye uchunguzi au Pengine ni kweli kalewa. Mwenyezimungu awape familia yake moyo wa subra kwenye wakati mgumu Kama huo na imani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...