Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi,Mh.Mwigulu Lameck Nchemba akisikiliza kero za wadau wa machinjio ya Vingunguti usiku  wa January 01/01/2016.Mwigulu Nchemba akishuhudia Ng'ombe aliyetayari kwa taratibu za kuchinjwa kwa ajili ya kitoweo.
Mbuzi wakiwa tayari kwa ajili ya kuchinjwa kwenye machinjio hayo ya Vingunguti.Mbuzi hawa asilimia kubwa wanatoka mnada wa Pugu ambao Ushuru wake unakusanywa na serikali kuu.Waziri Mwigulu Nchemba akikagua maeneo ya machinjio hayo usiku huu.
Mwigulu Nchemba akitoa maagizo kwa uongozi wa Machinjio ya Vingunguti kukutana kesho saa 2:00 asubuhi kwa wahusika wote wenye dhamana na Machinjio hayo,Mkutano utafanyika eneo la Machinjio hayo.
----------------------------------

Katika hatua ya kushitukiza,Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh.Mwigulu Nchemba amefanya ukaguzi wa Machinjio ya Vingunguti usiku wa Ijumaa Januari 1, 2016.
Mh.Mwigulu Nchemba amefika kwenye Machinjio hayo usiku huo ilikushuhudia Mifugo ikiandaliwa kwa ajili ya kitoweo cha wananchi.Uchinjaji wa Ng'ombe na Mbuzi katika machinjio haya hufanyika nyakati za Usiku kuanzia saa 4 hadi 10 alfajiri.
Mbali na kusikiliza kero na maoni ya wananchi kuhusu uendeshwaji wa Machinjio hayo,Mwigulu Nchemba ameshuhudia utafunwaji wa kodi ya serikali inayokusanywa kwenye mnada wa Pugu.
Utafunwaji huo unatokana na uandikaji wa kibali cha mifugo michache kuja Machinjioni ili hali mifugo zaidi huingizwa machinjioni bila kibali.
Mathalani  Mh.Waziri ameshuhudia Ng'ombe waliotoka mnada wa Pugu ambao wameshalipiwa kodi wakiwa 1450 lakini kibali chake kimeandikwa Ng'ombe 300 tu.Ikimaanisha kuna ng'ombe 1150 wamelipiwa ushuru lakini machinjioni kimeletwa kibali cha ng'ombe 300 wakati kwa hesabu ng'ombe hao wanazidi 1000.
Kutokana na hali hiyo,Mh.Waziri ameagiza wahusika wote kufika kesho kwenye mkutano wa asubuhi kwa ajili ya hatua stahiki kuchukuliwa.
Mhe Mwigulu amesisitiza kuwa kwa mtu yeyote mwenye dhamana na kusimamia sekta ya kilimo,Mifugo na Uvuvi afanye kazi  kwa mujibu wa sharia,vinginevyo hakutakuwa na huruma kwa wanaohujumu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Asante baba hayo ndio tuyatakayo kwenye hii serikali rushwa mwiko na ufisadi haikubaliki kabisa waambie wazipe zote hizo pesa walizo fuja ndugu zangu watanzania msituke hii ni serikali ya awamu ya 5 chini ya Rais Magufuli hakuna mchezo na pesa za watanzania

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...