Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Jordan Rugimbana kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Wazee na Watoto amezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya uhamasishaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii ( CHF) katika kata ya Nyangamara iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini.

Katika uzinduzi huo ulioratibiwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kushirikiana na Halmashauri ya Lindi Vijijini kaya zipatazo 261(sawa na wanufaika 1,566) zilisajiliwa papo hapo katika CHF kwa mchango wa Shilingi 10,000 kwa mwaka. Pia Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Nawanda alihamasisha viongozi mbalimbali wa Mkoa huo ambao hawakuwepo ambapo zilichangwa fedha kwa ajili ya kaya 2,060 za watu wasio na uwezo ili waandikishwe katika CHF.

Katika uchangiaji huo Mh. Waziri Mkuu ambaye ni Mbunge wa Ruangwa alichangia usajili wa kaya 900 ambapo Mkuu wa mkoa wa Lindi Mh. Rugimbana alichangia kaya 100, RAS Lindi - kaya 100, DC Lindi - kaya 50, NHIF kaya 300, Mh. Waziri wa Habari na Mbunge wa Mtama - kaya 300, Mh. Lalinda Mbunge wa Viti maalum CUF - kaya 50, Mh. Hamida viti maalum CCM - kaya 60, Mh. Hamid Bohali Mbunge wa Mchinga - kaya 100, Mh. Kaunje Mbunge wa Lindi - kaya 100.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Lindi akikabidhi kadi ya CHF kwa mnufaika mpya wa CHF Bw. Hassan Namangaya wakati wa Uzinduzi. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa CHF Bw. E. Mikongoti alisema mkoa wa LIndi una wanufaika 89,836 wa CHF ambayo ni asilimia 6.6 ya wana Lindi. Alihimiza Mkoa kuifanya CHF kuwa agenda katika utekelezaji mkoani hapo lakini pia kutumia vema fedha za uchangiaji ili kuboresha huduma za afya ili kuvutia wengi zaidi kujiunga na Mfuko huo. 

Wakati akiwasilisha ripoti ya CHF mkoa wa Lindi, Mganga Mkuu wa mkoa Dk. Sonda alisema Lindi imefanikiwa kupata malipo ya Tele kwa Tele ya CHF ya SHilingi 109,436,000 kwa mwaka 2015 ambazo ni mchangi mkubwa katika kuboresha afya mkoani humo. Hata hivyo aligusia kusema bado wana changamoto ya hamasa ya watendaji kuhusu CHF.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...