Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Profesa Makame Mbarawa akipokea taarifa ya Utendaji kutoka kwa Mkurugenzi wa Biashara na Maendeleo wa kitengo cha huduma ya Makontena Bandarini (TICTS) Bw.Donald Talawa mara alipofanya ziara ya kukagua utendaji wa kitengo hicho Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Viongozi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na TICTS ambapo amehimiza kuhusu hutoaji wa huduma kwa haraka ili kuongeza ukusanyaji wa mapato,Kulia ni Hebel Mhanga na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bwana Aloyce Matei.
Mtaalamu wa Uratibu wa huduma za upakuaji wa TICTS akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Mbarawa (Wa tatu kushoto) jinsi ya mfumo wa kupokea na kupakua Makontena unavyfanya kazi.
Wafanyakazi wa TICTS wakiendelea na utekelezaji wa majukumu yao ya kupokea na kuruhusu makontena.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Viongozi wa vitengo vya bandari wamulikwe zaidi. Huchelewesha kutoa mizigo maksudi ili mteja atoe fedha za ziada. Kwa nini kutoa mzigo zisiwe siku 2 tu? Watu wengi wataitumia bandari na serikali itakusanya kodi nyingi zaidi na kujaza mabilioni kwa miradi ya maendeleo.

    ReplyDelete
  2. Moja ya mikataba mibovu kupita maelezo, ukijawa na harufu ya uvundo wa ufisadi, ni mkataba kati ya serikali na TICTS. AIBU! Inasemekana kwamba nchi nyingi duniani huwa hazibinafsishi kitengo cha upakuaji makontena bandarini kwani ndicho chenye mapato makubwa na ni rahisi kukisimamia na kukiendesha! Huwa najiuliza hivi mikataba ya aibu kwa taifa ambayo tuliingia wakati wa Mkapa hamna clause inayoipa serikali kurudi mezani ili kuirekebisha kwa maslaji ya taifa!?

    Wakati nikifurajishwa na kasi ya Magufuli nasubiri kuona atachukua hatua gani kurekebisha mikataba mibovu ambayo ikirekebishwa ni uhakika baada ya miaka michache tu hatutohitaji misaada vitanzi toka ughaibuni. Kwa maoni yangu, wala Magufuli hahitaji kututangazia bali anaifanya kimya kimya kwa kuwaita na kuwapa terms mpya, serikali inamiliki 50-70%, wawekezaji wa nje wanapata 0.001-45%, wakiwa wa ndani wanafika mpaka 55%.

    Alafu kwenye ardhi hamna kutoa lease zaidi ya miaka 25 (renewable) kwa wawekezaji wa nje. Kwa sasa wapo wenye lease za mpaka miaka 99!

    Naamini Magufuli anawavutia kasi, muda utafika! Mungu ampe ujasiri na AMLINDE ili aweze kutenda bila woga! Nawasilisha

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...