Na Magreth Kinabo –Maelezo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, jinsia,
Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema misaada inayotolewa na watu mbalimbali kwa
ajili ya kusaidia jamii ni lazima iwe imekidhi viwango vya ubora, hivyo
haitakiwi kuangaliwa kwa vigezo vya dini, itikadi wala siasa.
Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu
huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake baada kituo
kimojwapo nchini kukataa misaada iliyotolewa na Mbunge wa
Bukoba Mjini (Chadema), Wilfred Lwakatare wa Chama cha Wananchi(CUF), hivi
karibuni.
Dkt. Ulisubisya alisema hivi karibuni gazeti moja la kila
siku la hapa nchini liliripoti kwamba misaada iliyotolewa na Mbunge huyo,
katika baadhi vituo afya Zahanati kwa
ajili ya wajawazito kukataliwa.
“Serikali ina sera ya kusaidia jamii hususan misaada inayotolewa kwenye huduma za afya, ambayo inakidhi viwango vya ubora kulingana Sheria , kanuni na taratibu za Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA),” alisema Katibu Mkuu huyo.
“Serikali ina sera ya kusaidia jamii hususan misaada inayotolewa kwenye huduma za afya, ambayo inakidhi viwango vya ubora kulingana Sheria , kanuni na taratibu za Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA),” alisema Katibu Mkuu huyo.
Kwa mujibu wa chanzo kimoja cha habari kiliripoti kwamba
baadhi ya wakuu wa vituo vya afya na zahanati katika Manispaa ya Bukoba,
wamegoma kupokea misaada kwa ajili ya wajawazito uliotolewa na kwa madai ya
kupewa maelekezo na Serikali.Dkt. Ulisubisya aliwataka watendaji wa afya wa vituo hivyo kuwa wasiangalie
misaada hiyo kwa misingi ya dini, itikadi na kisiasa.
Hata hivyo Katibu Mkuu huyo aliwataka watu mbalimbali wenye lengo la kutoa misaada katika vituo vya afya kuhakikisha kwamba imekidhi viwango viliyowekwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA). Katika hatua nyingine aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dkt. Donan Mmbando alikabidhi ofisi hiyo kwa Katibu Mkuu huyo mpya.
Hata hivyo Katibu Mkuu huyo aliwataka watu mbalimbali wenye lengo la kutoa misaada katika vituo vya afya kuhakikisha kwamba imekidhi viwango viliyowekwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA). Katika hatua nyingine aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dkt. Donan Mmbando alikabidhi ofisi hiyo kwa Katibu Mkuu huyo mpya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...