MWILI WA SWAI KUSAFIRISHWA LEO KWENDA KILIMANJARO
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) linapenda kuwajulisha wapenzi, wadau, wa mpira wa miguu nchini kuwa, mwili wa aliyekua Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Simiyu, Epaphra Swai utaangwa leo saa 9 alasiri katika hosiptali ya Muhimbili, na baadae saa 11 jioni itaanza safari ya kuelekea mkoani Kilimanjaro. Fuata link chini kwa taarifa zaidi

LIGI KUU KUENDELEA JUMAMOSI
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo saba kuchezwa katika viwanja tofauti, ikiwa katika mzunguko wa 16 kwa kila timu kusaka pointi 3 muhimu katika raundi hiyo ya lala salama. Fuata link chini kwa taarifa zaidi

STARTIMES RAUNDI YA 12 WIKIENDI HII
Vita ya kuwania kupanda daraja msimu ujao itaendelea wikiendi hii kwa michezo 12 ya Ligi daraja la kwanza nchini (Startimes League) kuchezwa katika viwanja mbalimbali kwa makundi A, B, C, kwa kila timu kusaka pointi tatu muhimu. Fuata link chini kwa taarifa zaidi

SDL KUENDELEA WIKIENDI
Ligi Daraja la Pili nchini (SDL) mzunguko wa pili unatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini, kwa timu nne za juu kutoka makundi A, B, C na D kusaka kupanda daraja msimu ujao. Fuata link chini kwa taarifa zaidi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...