Mwanaharakati wa mabalozi wa usalama barabarani na ASASI YA WAZALENDO NA MAENDELEO TANZANIA Bw. Ally Nurdini Six anasikitika kutangaza kifo cha Baba yake mzazi marehemu mzee Hassan Nurdin (R.I.P) aliyefariki  majira ya saa 9.00 alasiri siku ya Ijumaa tarehe 08 Januari,  2016 mjini Moshi.

Habari ziwafikie ndugu, jamaa, marafiki na majirani popote pale walipo.

Marehem Mzee Hassan Nurdin alikuwa ameugua kwa muda wa miezi sita, ambapo mtoto wake mkubwa Bw. Ally Nurdin Six alichukua likizo kuungana na familia mjini Moshi kwa ajili ya kumuuguza mzazi wake. Lakini Mwenyezi Mungu akamchukua kiumbe wake.

Mazishi yantarajiwa kuwa Saa 7 mchana siku ya Jumapili tarehen 10 Januari 2016 katika makaburi ya Njoro, Moshi Mjini, baada ya Marehemu kuswaliwa katika Msikiti kwa Mtei ambao uko jirani na CCM kata ya Mji Mpya Mchomba Centre.

Mwenyezi Mungu ampumzishe amlaze 
mahala pema peponi marehemu
AMINA.
Inna Lillahi wa inna Raji'un'

Kwa maelezo zaidi na  Rambi rambi wasiliana na:
Ally Six Nurdin
au Chief Daudi Mrindoko

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...