Na Asteria Muhozya, Arusha
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imetoa wito kwa wawekezaji wa ndani na nje katika Sekta ya Madini kuwekeza katika kuanzisha Vituo vya Uongezaji Thamani Madini ili kuendeleza fani hiyo kwa manufaa ya uchumi wa taifa.
Wito huo umetolewa leo jijini Arusha na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Sekta ya Madini, Profesa James Mdoe wakati wa Mahafali ya Pili katika fani za Ukataji na Unga’rishaji Madini ya Vito katika Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGDC).
Profesa Mdoe amesema kuwa, uongezaji thamani madini unalenga kuongeza fursa za ajira, kwa Watanzania watakaofanya kazi katika vituo hivyo, ikiwemo pia kutoa fursa za wataalamu wa sekta hiyo kujiajiri na hivyo kuongeza mapato kwa Serikali jambo ambalo pia litasaidia kuongeza mchango wa sekta hiyo katika Pato la Taifa.
Ameongeza kuwa, Kituo hicho kina historia ya ya pekee katika historia ya sekta ya Madini kwa kuwa kimekuwa kituo cha kwanza na pekee kuanzishwa hapa nchini, na kuongeza kuwa, uwepo wake ni kielelezo sahihi cha kazi za ubunifu na uongezaji thamani madini ya vito.
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imetoa wito kwa wawekezaji wa ndani na nje katika Sekta ya Madini kuwekeza katika kuanzisha Vituo vya Uongezaji Thamani Madini ili kuendeleza fani hiyo kwa manufaa ya uchumi wa taifa.
Wito huo umetolewa leo jijini Arusha na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Sekta ya Madini, Profesa James Mdoe wakati wa Mahafali ya Pili katika fani za Ukataji na Unga’rishaji Madini ya Vito katika Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGDC).
Profesa Mdoe amesema kuwa, uongezaji thamani madini unalenga kuongeza fursa za ajira, kwa Watanzania watakaofanya kazi katika vituo hivyo, ikiwemo pia kutoa fursa za wataalamu wa sekta hiyo kujiajiri na hivyo kuongeza mapato kwa Serikali jambo ambalo pia litasaidia kuongeza mchango wa sekta hiyo katika Pato la Taifa.
Ameongeza kuwa, Kituo hicho kina historia ya ya pekee katika historia ya sekta ya Madini kwa kuwa kimekuwa kituo cha kwanza na pekee kuanzishwa hapa nchini, na kuongeza kuwa, uwepo wake ni kielelezo sahihi cha kazi za ubunifu na uongezaji thamani madini ya vito.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Sekta ya
Madini, Profesa James Mdoe akiangalia madini mbalimbali kupitia kifaa
kinachotumika kukuza mawe ya madini ili yaweze kuonekana vizuri ikiwemo
kubaini kasoro . Kabla ya kutunuku vyeti Wahitimu 14 wa Mafunzo ya
kunga’risha na kukata madini ya Vito, Prof. Msofe amepata fursa ya
kuangalia bidhaa mbalimbali za mapambo zilizotengenezwa na wahitimu hao
ikiwemo vifaa vinavyotumika wakati wa mafunzo. Anayemwonesha kushoto ni
Mtumishi katika cha Jimolojia Tanzania, Salome Tilumanywa (kushoto).
Wengine wa kwanza kulia ni Kaimu Mratibu wa Kituo hicho John Mushi,
anayefuata ni Kamishna Msaidizi wa Madini anayeshughulikia masuala ya
Uchumi na Biashara ya Madini, Salim Salim.
Pia amesema kuwa, kuanzishwa kwa kituo hicho ni moja ya hatua za
Serikali za kutimiza malengo yaliyomo katika Sera ya Madini ya Mwaka
2009 yenye lengo la kuongeza mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la
taifa na ajira kwa watanzania kupitia uongezaji thamani madini, ikiwa
pamoja na mafunzo ua Jemomojia, ukataji na unga’rishaji wa madini ya
vito , utengenezaji wa bidhaa za mapambo na uchongaji wa vinyago vya
mawe.
Aidha, Profesa Msofe ametoa wito kwa Kampuni zinazofanya biashara ya madini ya vito na wadau wengine kuchangia maendeleo ya Kituo hicho ili kiwe kitovu cha kutoa Wataalamu wanaokidhi mahitaji ya tasnia ya madini ya vito nchini.
Akizungumzia zuio la mwaka 2010 la kusafirisha Tanzanite ghafi inayozidi gramu moja nje ya nchi, amesema lengo la zuio hilo ilikuwa ni kuhamasiaha ujenzi wa vituo , vyuo, taasisi na viwanda vya kuongeza thamani ya madini hayo nchini na kuongeza kuwa, jambo hilo pia ndilo lililopelekea Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kuanzisha kituo hicho.
Aidha, Profesa Msofe ametoa wito kwa Kampuni zinazofanya biashara ya madini ya vito na wadau wengine kuchangia maendeleo ya Kituo hicho ili kiwe kitovu cha kutoa Wataalamu wanaokidhi mahitaji ya tasnia ya madini ya vito nchini.
Akizungumzia zuio la mwaka 2010 la kusafirisha Tanzanite ghafi inayozidi gramu moja nje ya nchi, amesema lengo la zuio hilo ilikuwa ni kuhamasiaha ujenzi wa vituo , vyuo, taasisi na viwanda vya kuongeza thamani ya madini hayo nchini na kuongeza kuwa, jambo hilo pia ndilo lililopelekea Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kuanzisha kituo hicho.
Mmoja
wa Walimu katika Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC), Ramadhan Haizer
(kushoto) akimwonesha mfano wa mapambo ya vito ambayo Wahitimu wamepata
mafunzo ya kutengeneza katika mikato mbalimbali katika fani za
Unga’rishaji na uchongaji madini ya vito Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, anayeshughulikia Sekta ya Madini, Profesa James (wa
pili kushoto). Katikati ni Kaimu Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi
Ally Samaje.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...