Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akizungumza na wananchi katika kijiji cha Chimwenga wilaya ya Mbeya vijijini ambapo Naibu Waziri aliwaeleza wananchi hao umuhimu wa kukaa mbali na vyanzo vya maji ili kutoviharibu na kusababisha upungufu wa maji unaopelekea bwawa la uzalishaji umeme la Mtera kukauka.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) na Mkuu wa wilaya ya Mbeya Nyirembe Munasa wakiwa katika kijiji cha Makwenji wilaya ya Mbeya vijijini ambapo Naibu Waziri alikagua vyanzo vinavyotiririsha maji kwenye mito inayopeleka maji katika bwawa la uzalishaji umeme la Mtera.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (mwenye tai nyekundu) akikagua moja ya miradi mikubwa ya kilimo cha umwagiliaji inayofanyika katika wilaya ya Mbarali mkoa wa Mbeya ambayo hutumia maji kutoka katika mapitio yanayopeleka maji katika bwawa la uzalishaji umeme la Mtera.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...