Watu wengi wamekuwa wakilalamika ifikapo Jumamosi wanakuwa wamechoka  kwa usiku wa jana yake yaani ijumaa, na wengine hushindwa kufanya shughuli zao muhimu kwa ufanisi siku ya Jumatatu sababu ya uchovu wa wikiendi,  je ni siku ipi nzuri kwa starehe?. JovagoTanzania inakupa njia sahihi za kufurahia wikiendi yako kuanzia Ijumaa mpaka Jumapili.
1.       Ijumaa
Hii ni siku ndani ya siku za kazi, baadhi ya watu humaliza kazi zao kuanzia saa sita mchana na ofisi nyingine hadi jioni.  Je ni muhimu kutoka siku hii?  Jibu ni inategemea na umuhimu wa siku ya kesho yake (Jumamosi) au jinsi ya mtoko uliouandaa.  Ukiangalia kwa undani zaidi hii siku nzuri sana kwa kupunguzia uchovu wote wa wikinzima kazini, unaweza kutoka na wafanyakazi wenzako sehemu mbali mbali za starehe,  lakini pia  ni siku nzuri ya kuikaribisha vyema siku ya pili yake ambayo ni Jumamosi, hivyo unashauriwa kama unakunywa kunywa kidogo sana, jaribu kufanya starehe ambayo haitakuchosha mwili wako mpaka ukashindwa kuamka siku nzima ya Jumamosi au ukashindwa kurudi nyumbani kabisa.

2.       Jumamosi
Jumamosi ni siku nzuri ya kutoka kwa mapumziko lakini pia kuna baadhi ya watu huenda kazini na kurudi mchana, jaribu kuitumia siku hii ipasavyo kwani ni siku nzuri kwa kupunguzia uchovu wote wa jana (Ijumaa)  na wa wiki nzima.  Wengi hupendelea kwenda ufukweni mida ya mchana na jioni, na usiku kwenda sehemu za muziki tulivu, sinema, mpira au kwenda mbali na mji kama Bagamoyo.  Lakini pia kama siku ya Jumapili ni muhimu kwako jali muda wako ifikapo usiku na aina ya starehe utakayoifanya.

3.       Jumapili.

Siku ya Jumapili itumike kwa umakini kwani huikaribisha siku ya kazi ambayo ni Jumatatu. Unaweza kuwa ulienda mbali na mji siku ya jumamosi, basi jaribu kurudi mapema nyumbani. Pia ni siku nzuri kwa sinema, mpira na kupiga stori nyumbani au kutembelea ndugu na marafiki. Hakikisha siku hii haikuharibii siku ya kazi ambayo ni Jumatatu, bali ikupe uhuru wa kurudisha nguvu zako kazini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...