Picha za mitambo ya kuzalisha umeme na  wadau wa maji waliotembelea maeneo ya mito na kugundua baadhi ya njia za asili za  mito inayomwaga maji yake kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme imezibwa.  kitendo hicho kinadaiwa kuathiri utiririshaji wa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme.

 pia wadau hao wameshauri taasisi zote ikiwemo wizara ya nishati na madini,wizara ya kilimo , mifugo na uvuvi, wizara ya maji na umwagiliaji pamoja na bonde la mto Rufiji  zinazotumia rasilimali maji katika shughuli zake kushirikiana ili kumaliza tatizo la kukauka na kupungua kwa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme.
 Cable wire za Umeme zikipitishwa katika moja ya njia zililizopo chini ya  mwamba wa mlima( tannel) ambapo ndipo zilizopo mashine za kuzalisha umeme wa maji na shughuli zote za uzalishaji.
 Mashine  za kuzalisha umeme wa maji katika vituo vya Kihansi, kidato na Mtera  vinanyonekana ambapo shughuli zote za uzalisha wa umeme wa maji na mashine hizo ziko chini ya mwamba wa mlima uliotombelea . 
 Sehemu iliyochepushwa maji kitaalamu kutoka katika moja ya mito inayomwaga maji kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji ili maji hayo  yatumike kwa kilimo cha umwagiliaji.
 Sehemu iliyochepushwa maji kitaalamu kutoka katika moja ya mito inayomwaga maji kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji ili maji hayo  yatumike kwa kilimo cha umwagiliaji.
Wataalam kutoka Wizara ya Nishati  na Madini , Wizara ya kilimo ,uvuvi na mifugo, Wizara ya maji na umwagiliaji pamoja na watalaam kutoka bonde la mto Rufiji wakipita eneo ambalo kumejengwa tuta ili kuzua njia ya asili ya moja ya mito inayomwaga maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji kwa nia ya kupisha ujenzi wa mfereji wa maji yatakayotumika katika kilimo cha umwagiliaji, jambo ambalo  limedaiwa kuwa huathiri mazingira na utiririshaji wa maji katika mabwawa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mbona Mazingira mumewasahau wakati wao ndiyo wahusika wakuu katika utunzaji wa vyanzo vya maji?

    There are a number of initiatives zinafanyika Kihansi kuhusu utunzaji wa vyanzo vya maji lakini they are not involved.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...