Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Emmanuel Kalobelo akipokea nyaraka  kama ishara ya kukabidhiwa rasmi ofisi kutoka kwa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Inj. Ngossy Mwihava, wakishuhudiwa na Katibu Mkuu, Inj. Mbogo Futakamba.

Wizara ya Maji imemuaga rasmi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Inj. Ngossy Mwihava na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu mpya, Inj. Emmanuel Kalobelo katika Makao Makuu ya Wizara hiyo Ubungo Maji jana.


 “Naomba ushirikiano wenu ili tuweze kufanikisha azma ya kuleta maendeleo kwenye Sekta ya Maji, na nasisitiza kufanya kazi kwa bidii na kujituma kwetu sote ili tulete faraja kwa wananchi”, alisema Naibu Katibu Mkuu, Inj. Emmanuel Kalobelo katika hafla fupi ya kutambulishwa na makabidhiano ya ofisi.
 Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Ngossy Mwihava akizungumza na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Emmanuel Kalobelo ofisini kwake, kabla ya kumkabidhi ofisi.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Mbogo Futakamba (katikati), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Emmanuel Kalobelo (kushoto), aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Inj. Ngossy Mwihava (kulia) na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Gideon Manambo.
 Naibu Katibu Mkuu, Inj. Emmanuel Kalobelo akizungumza na Menejimenti ya Wizara ya Maji mara baada ya kutambulishwa.
 Menejimenti ya Wizara ya Maji ikimsikiliza Katibu Mkuu, Inj.  Mbogo Futakamba alipokuwa akizungumza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...