Dk. Mahadev, mshauri mwandamizi wa
radiotherapia kutoka Hospitali za Apollo.
Matibabu ya kawaida ya saratani huwa yanahusisha upasuaji, radiotherapia na kemotherapia. Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa kwenye tiba kwa njia hizo mbili. Katika hatua za mwanzo, saratani huwa ni ugonjwa unaotibika kwa dozi moja mahususi lakini saratani iliyosambaa au kukomaa inahitaji dozi zaidi ya moja katika kuitibu. Radiotherapia, ni tiba iliyopo katika mfumo maalumu unaoleta matokeo katika mwili mzima.
Dk. Mahadev , mshauri mwandamizi wa tiba ya uvimbe kwa mionzi kutoka hospitali za Apollo anaeleza kwamba radiotherapia inahusisha chembe chembe ndogo za mionzi ya gamma au X-rays katika kutibu saratani na hata matatizo ambayo sio ya saratani pia. Mionzi hii imegawanyika katika ile mionzi ya mbali (external radiotherapy) ambayo chanzo cha mionzi kinakuwa mbali na mwili na ile mionzi ya karibu ambayo mionzi inawekwa karibu ili kuchoma sehemu yenye uvimbe peke yake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...