Mkuu wa Itifaki na Mawasiliano wa Jiji la Dar es Salaam Gaston Makwembe, akizungumza na wandishi wa habari (hawapo picha)  leo jijini Dar es Salaam, juu ya mradi wa kuboresha jiji unagharimu sh.milioni 500 ambao unatarajia kuanza Julai Mwaka huu,kulia ni Mkuu wa Idara ya Udhibiti Taka Protus Membe. 
Wandishi wahaba habari wakimsikiriza Mkuu wa Itifaki na Mawasiliano wa Jiji la Dar es Salaam Gaston Makwembe.
(Picha na Emmanue Massaka wa Globul ya Jamii)


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
HALMASHAURI ya Jijin la Dar es Salaam kutengeneza jiji katika ubora (Smart Area) ikiwamo kuondoa biashara zisizo rasmi katikati ya jiji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Mkuu wa Itifaki na Mawasiliano wa Jiji, Gaston Makwembe amesema kuwa mradi huo wa kuboresha jiji unagharimu sh.milioni 500 ambao unatarajia kuanza Julai Mwaka huu.

Makwembe amesema katika uboreshaji huo utakwenda sambasamba na uondoaji wa ombaomba katika ya jiji la Dar es Salaam.

Maeneo yatakayoguswa ni barabara ya Kawawa kutoka makutano ya Kawawa na Karume hadi makutano ya Kawawa na Ali Hassan Mwinyi ,Makutano ya Mandela na Pungu pamoja maeneo ya mjini na Uwanja wa Ndege.

Makwembe amesema katika uboreshaji huo ni pamoja na uzuiaji wa Pikipiki,bajaji,Maguta pamoja na gari zinazozidi tani 10 kuingia katikati ya jiji.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...