Mtangazaji idhaa ya Kiswahili BBC London Maryam akimfanyia mahajiano nguli wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin jijini London siku ya Ijumaa Februari 12, 2016 mahojiano maalum kwa ajili ya Lady in Red itakayofanyika leo Jumamosi Februari 13, 2016 mjini humo. Onyesho hilo litakalo washirikisha wasanii mbalimbali wakiongozwa na msanii wa Bongo Flava Rich Mavoko litakua ni sehemu ya kusherehekea siku ya wapendanao ambayo mwaka huu imeangukia siku ya Jumapili.
 Kulia ni ClubMalibu ambaye ndiye mwenyeji na mdhamini wa Lady in Red itakayofanyika leo jijini London akiwa katika picha ya pamoja na mtangazaji mahiri wa idhaa ya Kiswahili BBC London Bwn. Salim Kikeke.
Kutoka kushoto ni msanii wa Bongo Flava Rich Mavoko, Mgalula Fundikila, Salim Kikeke na mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini walipokua mjengoni idhaa ya Kiswahili BBC London.
 Mtangazaji wa idhaa ya Kiswahili BBC London Sakuma Kssim akiwa katika picha ya pamoja na nguli wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin wakati mwanamitindo huyo alipokua mjengoni huko kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano.
 Kutoka kushoto ni Saluma Kassim, Maryam, Aisha Yahya wakiwa katika picha ya pamoja mama nguli wa mitindo Asya Idarous Khamsini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...