Februari 12, 2016), Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga akiambatana na baadhi ya viongozi wa Tume hiyo ametembelea Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wake, Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva kuhusu uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Katika ziara hiyo, Mhe. Nyanduga alipata fursa pia ya kumweleza Mhe. Lubuva kuhusu uangalizi uliofanywa na Tume katika uchaguzi huo katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Lindi na Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva akieleza jambo mbele ya ujumbe wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hauko pichani), ujumbe huo ulipoitembelea ofisi yake jana (Februari 12, 2016).
Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Bahame Tom Nyanduga na Katibu Mtendaji wa Tume, Bibi Mary Massay wakimsikiliza kwa makini Mhe. Jaji (Mstaafu) Lubuva.
Mhe. Jaji (Mstaafu) Lubuva akimsikiliza Mhe. Nyanduga (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Bahame Tom Nyanduga na Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva wakiwa katika picha ya pamoja na Kamishna wa Tume, Mhe. Dkt. Kelvin Mandopi na Bibi Mary Massay.
Mhe. Bahame Tom Nyanduga na Mhe. Jaji (Mstaafu), Damian Lubuva wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa THBUB na baadhi ya maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
(Picha zote na Germanus Joseph wa THBUB).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...