Na Mugishagwe Zablon
Walimu wa shule za msingi binafsi za jijini Dar es Salaam
jana wameanza mafunzo kuhusiana na mitaala mipya ya masomo kufuatia mabadiliko
yaliyofanywa na serikali hivi karibuni ambayo sasa yanafanya elimu hiyo iwe
hadi darasa la 10 badala ya la saba la awali.
Akizungumza wakati wa
kufungua mafunzo ya ufundishaji kwa walimu kwa kutumia mtaala ulioboreshwa kwa
wanafunzi wa darasa la kwanza na pili kwa shule binafsi, Kamishna wa Elimu
katika Wizara ya Elimu, Teknolojia, Sayansi na Ufundi, Profesa Eustella Balalusesa
alisema lengo ni kuboresha kiwango cha elimu nchini.
Kamishna huyo alisema mtaala huo uliofanyhiwa maboresho
umeanza kutumika katika shule za msingi nchini na kinachofanyika hivi sasa ni
mafunzo kwa walimu hao ambayo alisema kuwa ingawa yamechelewa lakini bado
yanahitajika.
Alisema ingawa walimu wa shule za msingi za serikali
wamepata mafunzo hayo lakini wale wa binafsi walikuwa bado na sasa ndio wakati
wao lengo kuhakikisha kunakuwa na uwiano wa viwango vya elimu baina ya shule na
pia kuwa na mtaala mmoja.
Kamishna huyo alibainisha kuwa licha ya mitaala hiyo ya la
kwanza na la pili kukamilika pia imeandaliwa ambayo imetayarishwa kwa lugha ya
kiingereza na Kiswahili ili kukidhi mahitaji ya shule zote iwe za serikali au
za binafsi.
Alisema pia kulingana na mabadiliko hayo, pia kutakuwa na
mitihani ya kuwapima wanafunzi wa darasa la pili ili kuzuia uwezekano wa kuwa
na darasa la tatu wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu ili kujua uwezo wa
watoto kitaaluma na kuwasaidia wale ambao uwezo wao mdogo katika eneo hilo.
Pia vitabu vyote vya kiada kwa shule za msingi vitachapisha
na kusambazwa na TIE “Msingi wa utungaji, uchapaji na usambazaji wa vitabu vya kiada
kwa shule za msingi nchini unatokana na kauli ya Rais John Magufuli ya kutaka
vitabu vya masomo msingi nchini kuchapwa na taasisi hiyo ili kudhibiti upotoshaji na kuhuisha elimu
nchini” alisema.
Profesa Balalusesa alisema kinachofanyika sasa sio kuandika
mtaala mpya isipokuwa kuufanyia maboresho ule wa mwaka 2005 ili uendane na
mabadiliko ya sasa ambayo yanataka elimu msingi iwe hadi darasa la 10 badala ya
la saba
Alibainisha kuwa awali ulikamilika mtaala wa darasa la
kwanza na pili na hivi karibuni wa la tatu na nne na itaendelea hivyo hadi
kufikia kulikokusudiwa ambako ni kuwa na mtaala ambao utaunganisha elimu ya
msingi na sekondari kabla ya kuelekea hatua zaidi.
Awali akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo, Ofisa
Eimu Wilaya ya Ilala, Elizabeth Thomas alisema wilaya ya Ilala imeamua
kuwashirikisha waimu wa sule binafsi pia kutokana na ukweli kuwa ni wadau
wakubwa wa elimu hususan jijini Dar es Salaam.
Ofisa
Eimu Wilaya ya Ilala, Elizabeth Thomas akizungumza wakati wa semina ya mafunzo kwa
walimu ya jinsi ya kufundisha kwa kutumia mtaala ulioboreshwa kwa shule za msingi kutokana na mabadiliko ya
sasa ambako wanafunzi watasoma hadi darasa la 10 badala ya la saba kama
ilivyokuwa awali ambayo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.
Katibu
Mkuu wa Chama cha Wawekezaji Binafsi katika Elimu (TAPIA), Albert Katagira
akizungumza akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo kwa walimu wa
shule binafsi, jinsi ya kufundisha kwa
kutumia mtaala ulioboreshwa wa shule za
msingi kutokana na mabadiliko ya sasa ambako wanafunzi watasoma hadi darasa la
10 badala ya la saba, iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Walimu
wa shule za sekondari za binafsi, wakifuatilia semina ya mafunzo kwa walimu jinsi
ya kufundisha kwa kutumia mtaala ulioboreshwa
wa shule za msingi kutokana na mabadiliko ya sasa ambako wanafunzi
watasoma hadi darasa la 10 badala ya la saba, iliyofanyika jijini Dar es Salaam
leo.
Kamishna
wa Elimu katika Wizara ya Teknolojia, Sayansi na Ufundi, Profesa Eustella
Balalusesa akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo kwa walimu wa
shule binafsi, jinsi ya kufundisha kwa kutumia mtaala ulioboreshwa wa shule za msingi kutokana na mabadiliko ya
sasa ambako wanafunzi watasoma hadi darasa la 10 badala ya la saba,
iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Picha zote na Mugishagwe Zablon
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...