Benki ya CRDB inajivunia mapinduzi makubwa katika sekta ya fedha nchini, iliyoyafanya katika kipindi cha miaka 20 ya uwepo wake, kwa kufanikisha kuwafikishia huduma za kifedha Watanzania walio wengi na haswa walio vijijini, hivyo CRDB kujikuta imetimiza malengo ya kuanzishwa kwake.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dr. Charles Kimei, katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi, katika kutathimini mafanikio ya benki ya CRDB kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Benki ya CRDB.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dr. Charles Kimei, akifanya mahojiano maalum na Mwandishi wa Habari wa Kujitegemea, aliyejikita katika kuandika habari za kimaendeleo, Pascal Mayalla, kuhusiana na maendeleo yaliyoletwa na CRDB Banki katika kipindi cha miaka 20.
Dr Kimei amesema, miongoni mwa mafanikio makubwa ya kujivunia ya Benki ya CRDB, ni kitendo cha benki hiyo kufanikiwa kutimiza malengo, dira na dhima ya benki hiyo, ambayo ni kufikisha huduma za kibenki kwa Watanzania wengi zaidi hadi vijijini, ambapo lengo hili limetizwa kupitia kwa mawakala wa CRDB waitwao Fahari Huduma waliotapakaa nchi kote hadi Vijijini.
“Katika mambo mengi ambayo CRDB inajivunia katika miaka hii 20, ni kuingiza mfumo mpya wa kimapinduzi wa kutolea huduma kwa wateja wetu wengi zaidi hadi wa hali ya chini ambao wengi wako vijijini, wamekuwa hawafikiwi na huduma za kibenki, hivyo Lengo na azma ya CRDB ya kuwafikia wateja wengi, limetimizwa.
Akinamama wa Kibamba, wakielekea kwenye kituo cha Wakala wa Fahari Huduma wa Kibamba, kupata huduma za kifedha, wakala huo, unaomilikiwa na Bw. Frank Mwalinga na mkewe Mainda, wakati wa ziara za kukagua mafanikio ya miaka 20 ya Benki ya CRDB.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...