Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco) limeendelea kufanya operesheni maalumu ya kubaini wezi wa Maji na waharibifu wa miundombinu kwenye maeneo tofauti ya jijini humo na kubaini wizi mkubwa wa Maji eneo la Manzese Uzuri.

Katika msako huo uliofanyika juzi katika mtaa wa Chakula bora ,Manzese Uzuri , Dawasco ilibaini kuwepo kwa pampu kubwa mbili za kuvuta Maji zilizofungwa kwenye mabomba ya kupeleka Maji kwa wateja kinyume cha sheria.

Akizungumza kwenye tukio hilo Meneja wa Dawasco Magomeni, Mhandisi Pascal Fumbuka alieleza kuwa walipata taarifa za wizi wa Maji kutoka kwa wasamaria wema jinsi Maji yanavyouzwa kiwizi nyuma ya baa inayoitwa Migombani ambapo mmiliki wa eneo hilo aitwaye Donald Shirima alikimbia baada mafundi kutoka Dawasco kufika kwenye tukio.

“Tulipata taarifa ya wizi wa Maji kutoka kwa msamaria mwema, alitupa taarifa kuwa mwenye eneo alikuwa akiuza Maji kwa muda mrefu sana bila kuwa na mita kutoka Dawasco hivyo tulifika eneo la tukio “alisema Fumbuka.

Ofisa Mtendaji wa kata ya Manzese, Bi Salome Chilumba aliwasihi wananchi kuendelea kuwafichua  wezi wa Maji kwani hao ndio wanaofanya waliounganishiwa kihalali na Dawasco kukosa huduma hiyo. 

“Watu wanaohujumu huduma ya Maji kwa kujiunganishia kiholela hawafai ni lazima wote tushirikiane kuwafichua”,alisema Chilumba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...