![]() |
JAJI mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu (wa pili kulia) akifuatana na maafisa ya jeshi la Magereza Pemba wakati alipowatembelea mahabusu na wafungwa katika Gereza na Wete Pemba kufahamu matatizo mbali mbali yanayowakabili |
MRAJISI
wa Mahakama kuu Zanzibar Mhe. George Kazi (kulia) akichambua mambo mbali mbali
yanayofanywa katika Mahakama ya mwanzo Wete
AFISA
wa kitengo cha komputa (IT) Mahakama za Pemba Mohamed Juma (kulia)
akimfahamisha jambo Jaji mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu, juu ya
utendaji kazi wa komputa za Mahakama ya Wete wakati wa ziara yake Mahakamani hapo
MKURUGENZI
wa baraza na mji Wete Mgeni Othman aliyesimama akielezea matatizo mbali mbali
yanayoikabili Mahakama ya Mwanzo Wete, wakati jaji mkuu wa Zanzibar alipofanya
ziara Mahakamani hapo
AFISA
Mdhamini Wizara ya Ardhi, Maji, Makaazi na Nishati Pemba Hemed Salum Hemed akizungumzia
matatizo mbali mbali yanayoikabili Mahakama ya ardhi Wete, wakati wa ziara ya
jaji mkuu katika Mahakama hiyo. Picha zote na Picha
na Ameir Khalid
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...