Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt. Adelhem Meru amekutana ujumbe wa Jumuiya ya Mabohora kutoka Mumbai nchini India wenye lengo kuwekeza katika sekta ya Viwanda nchini.

Akizungumza katika mkutano huo Katibu Mkuu Dkt. Meru aliwakaribisha na kuwahakikishia uwepo wa mazingira bora na wezeshi kwa ajili ya uwekezaji Tanzania. “Tanzania ina malighafi nyingi kuanzia madini, mazao ya chakula, mbao, Samaki na kadhalika, tunawaomba mfike kwa wingi ili mje kuwekeza katika sekta ya Viwanda.”

Katibu Mkuu Dkt. Meru alisema dhamira ya Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha viwanda vinakuwa ni daraja la kubadilisha uchumi wa Tanzania kuwa wa kipato cha kati.

Alisema kuwa Sekta ya Viwanda ina jukumu kubwa la kuchangia pato la Taifa kwa asilimia 15 na vile vile kuongeza ajira kwa vijana hadi kufikia asilimia 40. “Kuwepo kwenu leo mahali hapa kunatia moyo ya kuona dhamira ya Serikali ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda inawezekana.”

Awali mwenyeji wa Jumuiya ya Mabohora nchini Bw. Murtaza Adamjee alimweleza katibu Mkuu lengo lao safari yao ni kuangalia fursa za uwekezaji katika sekta ya viwanda hususani.

Bw Adamjee aliongeza kuwa jumuiya hiyo itawekeza katika viwanda vya kutengeneza ngozi na viatu, nguo na mavazi, vifungashio, pamoja na viwanda vya chuma isiyoshika kutu.

Aidha Jamii ya Mabohora walitaka kuwepo na mawasiliano, kubadilishana uzoefu na ujuzi katika sekta ya viwanda na kuwaalika watanzania kutembelea India kuona maendeleo ya viwanda nchini India.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Adelhem Meru wa nne (kulia), Naibu katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Mhandisi Joseph Malongo wa tatu (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Jumuiya ya Mabohora kutoka nchini India waliotembelea wizarani mapema leo wakiwa na dhamira ya kuwekeza katika sekta ya Viwanda. Kulia kwa Katibu Mkuu ni Bw. Murtaza Adamjee Mkururugenzi wa kampuni ya Global Group ambaye pia ni mwenjeji wa ugeni huo.
Katibu Mkuu Dkt.Adelhem Meru akimsikiliza kwa makini Bw.Murtaza Adamjee alipokuwa akiwatambulisha wageni alioongozana nao katika ziara hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara akizungumza na vijana kutoka nchini India ambao wameonyesha nia ya kuwekeza katika sekta ya Viwanda.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Mhandisi Joseph Malongo, akimsikiliza kwa makini mmoja wawekezaji kutoka jumiya ya Mabohora waliotembelea Wizarani mapema hivi leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kwa wanaotaka kuwasiliana kwa biashara na wajumbe hao, tumia 0784 430 787 kwa ajili ya appointment. Wapo hadi mwishoni mwa wiki

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...