Mlinda Mlango wa Mbeya City, Juma Kaseja
Kocha mkuu wa Mbeya City Fc , Kinnah Phiri amesibitisha kuwa mlinda mlango mahiri wa kikosi  chake Juma  Kaseja  hatakuwa sehemu ya nyota watakaoiwakililisha Mbeya City kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania  Bara dhidi ya Simba Sports club uliopangwa kuchezwa  Jumapili hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar.

Muda mfupi uliopita kocha Phiri ameudokeza mtandao huu kuwa ilikuwa waungane na kipa huyo leo asubuhi kwenye kambi ya muda hapa Morogoro lakini imemlazimu kumuongezea muda zaidi wa kukaa  karibu na familia yake ili kushughulikia masuala kadhaa ya kifamilia aliyonayo hivi sasa.

“Wakati anaondoka Mbeya siku tano zilizopita tulikubaliana kuwa ataungana nasi hapa siku ya leo, nimezungumza nae leo asubuhi kuna mambo muhimu ya kifamilia amenieleza hivyo basi nimeamua kumuongezea siku  kadhaa za kubaki nyumbani kushughulikia  yale yote yaliyopo kwenye familia yake na imani yangu kuwa ataungana na kikosi mara tu tutakaporejea mbeya kujiandaa na mchezo dhidi ya Stand United March 10.

Juma  Kaseja aliondoka jijini Mbeya mara  baada ya mchezo wa Kombe la FA  dhidi ya Tanzania Prison  uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine kufuatia taarifa njema  ya mkewe kujifungua watoto mapacha.

Wachezaji wanzeke na uongozi wa City  kwa ujumla unampongeza Juma Kaseja na kumtakia  kila la kheri  kwenye malezi ya watoto wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...