MBUNGE wa Busanda (CCM) LOLENSIA BUKWIMBA ameeleza furaha yake kwa kamati maandalizi ya Tamasha hilo ambalo halikuwahi kufanyika mkoani humo na imekuwa faraja kwake kama mwakilishi wa wananchi  wa mkoa huo  unaokabiliwa na mauaji kwa walemavu wa ngozi.

Alisema amefurahishwa  kufanyika kwa tamasha hilo mkoani Geita na mikoa mgine kwani ana imani wakazi wa mkoa huo watahamasika  kuacha mauaji ya Watanzania wasio na hatia ambao ni walemavu wa ngozi na vikongwe ambayo yanaendelea. Mbunge huyo anaelezea furaha yake, ana imani wananchi wa mkoa wa Geita watafurahi kwa sababu mkoa huo umesuswa kwa kuwapelekea matamasha ya namna hiyo na kusikia yanafanyika katika mikoa mingine kama Dar es Salaam na Mwanza.

“Nimefurahi sana Msama kulileta Tamasha hili litakalopiga vita mauaji ya vikongwe na walemavu wa ngozi, nina imani wananchi wataweza kuelimika kwa njia moja au nyingine, baada ya hapo inawezekana kabisa likaweza kubadilisha fikra na mtizamo juu ya suala hili na kupunguza kabisa mauaji haya,” anasema Lolensia.

Alieleza kuwa limekuwa jambo la bahati kwa mkoa huo kufikiwa na tamasha hilo ambalo lina mafanikio makubwa katika kutimiza malengo yanayokusudiwa hivyo anaamini kilichokusudiwa kwa Geita kitafanikiwa kwa kiasi kikubwa. “Tunawakaribisha sana na nichukue nafasi ya pekee kumpongeza Msama kwa uamuzi wake wa kutuletea tamasha hili tunatarajia kupata mambo makubwa pia nina imani wanageita watafurahia mno kwasababu wanapenda mambo hayo ya muziki hasa huu wa Injili,” alisema Lolensia.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...