Leo Ijumaa Kuu Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela amezindua mafunzo ya watoto yanayo endeshwa na shirika la Compassion International (shirika la Shirika ka Kikistro ambalo lipo nchi 28 duniani, Shirika hili linahudumia zaidi ya watoto 4000 wa madhehebu yote mkoani Iringa. Mafunzo yatolewayo ni pamoja na;
1. Ulinzi wa Mtoto
2.Taarifa sahihi kuhusu VVU na UKIMWI
3.Ukombozi wa kiroho
4.Urafiki na urafiki wa siri
5.Ujasiliamali
6. Kulea maono
7.Stadi za Maisha
8. haki na wajibu wa Mtoto
9. Huduma na msaada wa Kisaikolojia
10. Kupambana na unyanyasaji na ukatili wa watoto.
Mhe Kasesela ametoa rai kwa wazazi kushiriki katika masomo na kulea vipaji vya watoto, na amewashauri waunde vikundi ambavyo vitawafundisha uongozi na ujasiliamali, ambapo kila kikundi kintakiwa kiwe na watoto 20. Pia amewaambia waandae wazo ambapo kikundi chenye wazo zuri kitapata zawadi ya shilingi laki 1. Vikundi 5 vyenye mawazo mazuri vitachaguliwa. Pia ameahidi kuhakikisha watoto wanalindwa.
"Ilikuwa siku nzuri sana kweli namshukuru MUNGU...", Mkuu huyo wa wilaya aliiambia Globu ya Jamii.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akizindua mafunzo ya watoto yanayo endeshwa na shirika la Compassion International shirika la Kikristo ambalo lipo katika nchi 28 duniani.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akishiriki mafunzo ya watoto yanayoendeshwa na shirika la Compassion International
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya watoto yanayoendeshwa na shirika la Compassion International
Irene Lyandala akisoma risala ya washiriki ya mafunzo hayo
Sehemu ya watoto wanaohudhuria mafunzo hayo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...