Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu ( Mb) akitoa hutuba kwa niaba ya Kundi la Nchi za Afrika wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 60 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hali ya Wanawake ( CSW).Mkutano huu wa wiki mbili unawakusanya wawakilishi kutoka serikali mbalimbali duniani na Asasi za Kiraia ambapo hujadiliana na kubalishana uzoefu na kuelimishana kuhusu hatua mbalimbali ambazo serikali zao zinachukua katika kuboresha maisha ya mwanamke na mtoto wa kike.
Waziri wa Malawi akimpongeza Waziri Ummy Mwalimu mara baada ya hotuba yake aliyoitoa kwa niaba ya Kundi la Nchi za Afrika.
Mhe. Waziri Mwalimu akichangia majadiliano ya Mawaziri yaliyofanyika mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa 60 wa Kamisheni kuhusu hali ya Wanawake. Majadiliano hayo ya Mawaziri yalihusu uimarishaji wa mfumo ya kisheria na kisera kwaajili na utekelezaji wa usawa wa jinsia na uwezeshaji wa wanawake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...