Afisa Mtendaji Mkuu wa Benjamin Mkapa Foundation, Dk. Ellen Mkondya Senkoro akiongea na waandishi wa habari kutangaza maadhimisho ya miaka kumi ya taasisi hiyo pamoja na shughuli mbalimbali zitazoambatana na maadhimisho hayo jijini Dar es salaam jana. Taasisi hiyo imekuwa kinara katika kuongoza jitihada za kuimarisha utoaji huduma za afya nchini katika miaka kumi iliyopita. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Programu za Taasisi hiyo Raheli Sheiza.
Taasisi ya Benjamin Mkapa (BMF) imeendelea kutekeleza kutekeleza jitihada za serikali ya Tanzania na washirika wake katika kuimarisha utoaji huduma za afya katika maeneo yasiyopata huduma ya uhakika na mwezi Aprili 2016, itaadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa Aprili 2006 na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniania, Mhe. Benjamin William Mkapa. 

 Afisa Mtendaji Mkuu wa BMF, Dk. Ellen Mkondya-Senkoro amesema kwenye mkutano na waandishi wa habari leo , kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya miaka kumi ni “Miaka 10 – Tumejituma, Tumeaminika na Tumeweza”. 

Taasisi ina furahia kuweza kubadilisha maisha na afya za mamilioni ya Watanzania ambao wamefikiwa moja kwa moja na ambao hawakufikiwa moja kwa moja ya Taasisi.

 Ameongeza kwamba “Ikiwa ni sehemu ya maadhimisho hayo, Taasisi ya Benjamin Mkapa itafanya shughuli mbalimbali za kijamii kuanzia March 2016 hadi mwisho wa Aprili 2016. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...