Mgeni rasmi,Waziri wa sheria na Katiba Dkt Harrison Mwakyembe akifafanua jambo mbele ya Wanahabari (hawapo pichani),kuhusiana na Ripoti ya maoni ya jumla kuhusu uchaguzi Mkuu uliopita,aliyoipokea kutoka kwa Waandaaji CEMOT (umoja wa taasisi za waangalizi wa ndani wa uchaguzi inayohusisha Kamati ya Uangalizi wa Uchaguzi (Temco) na Muungano wa taasisi zisizo za kiraia za kusimamia uchaguzi (Tacceo) ),kwenye semina iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Hyatt Hotel jijini Dar na kuwakutanisha Wadau mbalimbali wakiwemo Tume ya Uchaguzi (NEC),Polisi,PCCB pamoja na Nchi Wahisani .Pichani kushoto ni Mjumbe wa kamati ya CEMOT Bwa.Ezekiel Massanja
Katika mahojiano mafupi na Waandishi wa habari mara baada ya kuipokea ripoti hiyo,Dkt Mwakyembe alisema kuwa Ripoti hiyo iliangalia mapungufu yaliyokuwepo na namna ya kuyaboresha,Dkt Mwakyembe ametoa rai kwa Serikali,taasisi mbalimbali na wadau wengine waweze kuipitia ripoti hiyo na kujadiliana ili kuboresha chaguzi nyingine zinazokuja.
Wa pili kulia ni Mgeni rasmi,Waziri wa sheria na Katiba Dkt Harisson Mwakyembe akiandika jambo wakati ripoti ya maoni ya jumla kuhusu uchaguzi Mkuu uliopita,aliyoipokea kutoka kwa Waandaaji CEMOT ikisomwa.
Mkuu wa Waandaaji wa Ripoti ya maoni ya jumla kuhusu uchaguzi Mkuu uliopita (CEMOT),Dkt.Alexander Makulilo akisoma ripoti hiyo mbele ya Wadau na walioshiriki kuiandaa ripoti hiyo.
Baadhi ya Wadau walioshiriki kundaa Ripoti ya maoni ya jumla kuhusu uchaguzi Mkuu uliopita,wakifuatilia kwa makini wakati ripoti hiyo ikisomwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...